AKIBA
Chama hupokea na kutunza akiba za wanachama kupitia makato kwenye mshahara au mwanachama anaweza kulipa kupitia benki ;kiwango cha chini cha kila mwezi ikiwa ni Tsh 40,000/= kwa kila mwanachama.Aidha chama kinalipa riba 3%-7% ya akiba za mwanachama kila mwaka
HISA ZA HIARI NA LAZIMA
Kila mwanachama anatakiwa kununua hisa 40 @Tsh 10,000 ili kukamilisha uanachama wake.
AMANA(AMANA ILIYOWAZI)
Amana ni fedha ambayo mwanachama huweka kwa manufaa yake mwenywewe.Pia mwanachama anaweza kuweka na kuchukua mda wowote.
AMANA ZA MUDA MAALUMU
Hizi ni fedha ambazo mwanachama huweka kwa mda maalum na hawezi kuzitoa kutokana na makubaliano yaliyofikiwa baina ya chama na mwanachama.Amana maalum yaweza kuwekwa katika kipindi cha miezi mitatu(3),miezi sita(6),miezi tisa(9),miezi kumi na mbili(12).Faida katika amana maalum ni asilimia kumi(10%)kwa mwaka.